Header Ads

Afungwa Jela kwa Kutunga Shairi Kwenye uume wake Myanmar

Mwaandishi mmoja nchini Myanmar amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela, baada ya kutunga shairi kwa kuchora sura ya Rais wa zamani wa Myanmar, Thein Sein kwenye uume wake.
Maung Saungkha amehukumiwa kwa kosa la kumharibia mtu sifa mtandaoni baada ya kuchapisha shairi hilo katika mtandao wake wa kijamii wa Facebook.
Sasa akifahamika kama "penis poet", mtu huyo mwenye umri wa miaka 24 ataachiliwa huru baada ya kutumikia kifungo hicho cha miezi sita gerezani.
Mamlaka kuu nchini Burmer, inaendelea kuwafunga raia wake jela kwa kutoa maoni kwenye mitandao ya kijamii, ambayo yanaikosoa serikali hiyo.

No comments

Powered by Blogger.