Header Ads

Semina ya Kuwanoa Wadau wa Sekta ya Sanaa, yafanyika Jijini Dar es Salaam

Kwa mara ya kwanza, wadau wa Sanaa nchini wamepata fursa ya kukutana na Makampuni, Mashirika na Vyombo mbalimbali katika mafunzo yaliyofanyika hotel ya Hyatt Regency,jijini Dar es Salaam. Semina hii iliongozwa na Maria Sarungi Tsehai, ambaye ni mdau mkubwa katika sekta hii.

Mafunzo hayo yalifanywa na wataalam kutoka sekta mbalimbali kama Nyumba, Urembo, Saikolojia, Sanaa na Wasanii n.k....

Meneja Masoko wa Shirika la Nyumba, Arden Kitomari,akitoa mafunzo ya namna ya kuwekeza katika Sekta ya Nyumba nchini Tanzania,hususan kupitia miradi ya Shirika la Nyumba la Taifa.

Wadau wa Sanaa pia walipata mafuzo ya Namna ya kubalansi maisha yao ya Sanaa na yale ya Familia, kutoka kwa mwanasaikolojia maarufu, Aunt Sadaka Gandi.


Semina hii iliyopewa jina Celebrity Corporate Conference & Cocktail iliwahusisha pia COSOTA na BASATA ambao ni wasimamizi wakuu wa kazi za sanaa na taratibu zake.

Ms Doreen Anthony Sinare, CEO wa COSOTA akitoa somo kuhusu usajili wa kazi, masharti ya kuzingatiwa na Sheria zinazomlinda Msanii aliyesajiliwa.

Sekta lengwa katika semina hii ni wadau kutoka Filamu, Muziki, Urembo, Habari, na Wajasiriamali mashughuri.

Bwana Aristides kutoka BASATA aliwaelekeza wadau kuhusu Taratibu mpya za kujisajili na chombo hiki, pamoja na faida zake.


Je, Unafahamu namna ya kuifanya Talanta yako kuwa Biashara? Hii ndio ilikuwa mada iliyoongozwa na Mjasiriamali mashughuri, Shekha Nasser wa Shear Illusions.

Semina hii ya Celebrity Corporate Conference & Cocktail imeandaliwa na Kampuni ya Popular Links kwa udhamini wa Heineken, The Guardian, Nipashe, Leteraha, Hyatt Regency hotel, Ndovu Special Malt, Cocacola, NHC, COSOTA, Jamii Media, BASATA, Shear Illusions, Clouds Media na Slide Visuals.

No comments

Powered by Blogger.