Header Ads

Sherehe za Diwali zachafua Hali ya Hewa INDIA


Viwango vya uchafuzi wa hewa huko mjini Delhi nchini India vimeongezeka pakubwa hasa wakati wa usiku wa sherehe za jamii ya Wahindi, sherehe za Diwali, vikifikia mara 40 zaidi ya viwango vinavyopendekezwa na wataalam wa kimataifa, hayo ni kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO.

Hii ni kwa sababu ya kiwango kikubwa cha fataki ambazo zimekuwa kikifyatuliwa wakati wa shererhe hizo.

Kwa mfano Jumatano usiku vilifikia kiwango cha chembe chembe PM10 katika eneo lililopimwa ambacho ni hatari sana.

Kabla ya sherehe kuanza serikali ilikuwa imetoa wito watu wasitumie fataki katika sherehe hizo.

Gazeti la The Times of India hapo Jumatano lilikuwa limeripoti kuwa hali ya hewa imekuwa mbaya sana.

Viwango vya kemikali ya sulphur dioxide, ambayo inajulikana kuchochea pumu na maradhi mengine ya kupumua nayo pia ilikuwa ilikuwa juu katika maeneo mengi.

Uchunguzi wa WHO wa mwaka 2014 uligundua kuwa kati ya miji 20 iliyo na viwango vikubwa vya uchafuzi wa hali ya hewa duniani, 13 iko katika taifa la India, huku mji wa Delhi ukitajwa kushikilia nafasi ya kwanza ya miji iliyona uchafuzi zaidi wa hewa duniani.

Kuvuta hewa iliyo chafu imeorodheshwa kama mojawapo ya mambo yanayosababisha vifo vya mapema huko India, Takwimu zikionesha kuwa zaidiya watu 620,000 hufa kila mwaka kutokana na maradhi yanayochochewa na kupumua hewa iliyochafuliwa, WHO imesema.

Mambo mengine yanayoongezea uchafuzi wa hewa ni kuchomwa kwa maelfu ya tani za taka za mashambani, viwandani na hata taka za majumbani.

No comments

Powered by Blogger.