Header Ads

Waziri Mkuu KASSIM MAJALIWA afanya Ziara Kwenye Kiwanda cha Sukari MTIBWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Meneja wa Kiwanda cha sukari cha Kagera,  Ashuwin  Rana baada ya kuwasili kwenye  kiwanda  cha sukari cha Mtibwa  baada ya kuwasili kwenye kiwanda cha sukari cha Mtibwa Agosti 2, 2016. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Stephene Kebwe na wapili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha Kagera Sugar na Mtibwa Sugar, Seif  Ali Seif .
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza  baada ya kuwasili kwenye kiwanda cha sukari cha Mtibwa   kukagua uzalishaji  wa sukari katika kiwanda hicho, Agosti 2, 2016,   Kulia ni  mkewe Mary, wapili kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dkt. Stephene Kebwe na Wapili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha sukari cha Kagera na Mtibwa, Seif Ali Seif .  Kushoto ni Kaimu Katibu wa CCM mkoa Wa Morogoro, Kulwa Solobi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua eneo la mtambo wa maji ya kumwagilia katika shamba la miwa la kiwanda cha sukari cha Mtibwa  wakati alipokitembelea kiwanda hicho, Agosti 2, 2016.  Kushoto ni  mkewe Mary na wapili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha Sukari cha Kagera na Mtibwa, Seif  Ali Seif .
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha sukari cha Mtibwa wakati alipokitembelea kiwanda hicho Agosti 2, 2016.

(Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments

Powered by Blogger.