Header Ads

TAMADUNI ZETU; Wakurya na Sherehe za Uchinjaji wa Mbuzi Mkoani MARA

Kuna Sherehe za aina mbalimbali mkoani Mara, Leo mtandao huu unakujuza juu ya Shereze ya kuchinjiwa supu ya mbuzi, Hii hufanywa zaidi kwa wanajamii wa kabila la Wakurya mkoani humo.

Sherehe hizi hazina msimu maalumu bali hufanyika kadri familia moja na nyingine ama mtu na mtu walivyokubaliana, Mfano mtoto kumchinjia mzazi wake mbuzi kwa ajili ya supu (umusuri) au dada kumchinjia kaka ama mtu yeyote kulingana na makubaliano yao ambapo inaaminika mtu akiinywa supu hiyo husafisha tumbo.

Huchukuliwa kama Heshima kubwa pindi sherehe za aina hii zinapofanyika katika familia fulani ambapo ndugu, jamaa na marafiki hujumuika pamoja kama picha zinavyoonekana katika sherehe ya Chacha Kuchenga alipoenda kumchinjia mbuzi mdogo wake, Leah Marwa Binagi (Binti Kuchenga).

Supu huandaliwa...

Supu hii huchemshwa kwa masaa kadhaa bila kuungwa.

Muda wa kunywa supu.

Katika supu hiyo, huchanganywa damu mbichi ili kuongeza ladha.

Bonyeza  HAPA Kujua Zaidi.

No comments

Powered by Blogger.