Header Ads

RIPOTI MPYA : Tanzania Imepanda katika Uhuru wa Kiuchumi


Mkurugenzi  Mtendaji wa  Taasisi isiyo ya kiserikali inayojihusisha na  uboreshwaji wa sera za jamii kwa kutumia kanuni za Soko huria( UIPE)  Bw. Isack Danford katikati akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa mkutano wa kutoa tathimini ya uhuru wa kiuchumi jijini Dar es salaam leo wa kwa (kulia) ni Kiongozi msadizi Bi.  Morilyn Wambui na wa Kwanza Kushoto ni Mkuu wa kitengo cha sera Bw. Alexander Mtweve.

Mkurugenzi  Mtendaji wa  Taasisi isiyo ya kiserikali inayojihusisha na  uboreshwaji wa sera za jamii kwa kutumia kanuni za Soko huria( UIPE)  Bw. Isack Danford katikati akionyesha kitabu cha taarifa ya utafiti wa uchumi mbele ya waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa mkutano wa kutoa tathimini ya uhuru wa kiuchumi jijini Dar es salaam leo na wa Kwanza Kushoto ni Mkuu wa kitengo cha sera Bw. Alexander Mtweve.

Waandishi wa Habari wakimsikilza kwa makini Mkurugenzi  Mtendaji wa  Taasisi isiyo ya kiserikali inayojihusisha na uboreshwaji wa sera za jamii kwa kutumia kanuni za Soko huria( UIPE)  Bw. Isack Danford hayupo pichani  wakati wa mkutano wa kutoa tathimini ya uhuru wa kiuchumi jijini Dar es salaam leo.

(Picha na Ally Daud)




Na Skolastika Tweneshe na Mwanahamisi Matasi


Kwa mara nyingine tena, Tanzania imekuwa miongoni mwa nchi 100 duniani ambazo zipo huru kiuchumi kwa mujibu  wa ripoti ya (Economic Freedom of the World Report) ya mwaka 2015 itolewayo na umoja wa mashirika yasiyo ya kiserikali ujulikanao  kama Mtandao wa Kiuhuru wa Kiuchumi.


Hayo yamesemwa  na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika Huru lisilo la kiserikali linalojishughulisha na uboreshwaji wa Sera za Jamii (UIPE) Bw. Isack Danford alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo jijini  Dar es salaam ambapo amesema kuwa Tanzania imepanda kwa nafasi kumi  katika nafasi ripoti ya mwaka huu kutoka nafasi ya tisini na mbili katika ripoti ya mwaka 2014 hadi nafasi ya 82 katika ripoti ya mwaka 2015.


“Kwa sasa nchi yetu ya Tanzania inaendelea kupanda katika uhuru wa kiuchumi kwa kushika nafasi  ya 82 duniani na  nafasi ya tatu kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki  ikiishinda nchi ya Kenya ambayo  ilikuwa kinara miaka iliyopita“alisema Danford.


Mbali na maendeleo hayo zipo changamoto mbalimbali ambazo zinazobomoa uhuru wa kiuchumi Tanzania ni pamoja na malipo ya ziada(Extra payment), Hongo na upendeleo, gharama zitokanazo na urasimu na mahitaji ya kiutawala hii ni katika uthibiti wa biashara mbalimbali za ndani ya nchi.


Pia kwenye biashara za  kimataifa masuala yanayorudisha nyuma uhuru wa kiuchumi ni pamoja na vikwazo katika uwekezaji ,vikwazo visivyo vya kiforodha na tofauti katika viwango vya forodha.


Kwa mujibu wa tafiti wa watu waishio kwenye nchi zenye viwango vya  juu vya uhuru wa kiuchumi ripoti hii hupima uhuru wa kiuchumi wa  nchi mbalimbali  duniani kwa kutumia vigezo  vitano ambavyo ni, ukubwa wa serikali, sura ya kisheria, usalama  wa mali binafsi,fedha imara,uhuru wa kuifanya biashara kitaifa pamoja na udhibiti wa mikopo, ajira na biashara.


No comments

Powered by Blogger.