Header Ads

Zoezi la Kugawa Chakula Cha Msaada, Kambi ya Nyarugusu Mkoani KIGOMA Limeendelea

1
Wakimbizi kutoka nchini Burundi walioko katika kambi ya Nyarugusu wakiwa wamebeba shehena ya unga wa mahindi jana, muda mfupi baada ya kugawiwa chakula hicho Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia chakula (WFP), lililoweka kituo chake katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu wilayani Kasulu, mkoani Kigoma.

2
Byesige Josephat (anayemimina mafuta) na Hezron Mtangirwa (kushoto), wakimbizi kutoka Burundi waliohifadhiwa katika kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu wakipima mafuta ili waweze kuyagawa kwa wakimbizi wenzao jana,baada ya kugawiwa mafuta na Shirika la Umoja wa Mataifa, linaloshughulikia chakula (WFP), ambalo lina kituo chake katika kambi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma.

3
Kina mama wa kimbizi toka Burundi wakipata mgao wao wa unga unaotolewa kwa wakimbizi wanaohifadhiwa katika Kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Serikali kwakushirikiana na Mashirika ya Kimataifa imeendelea kuhakikisha kuwa wakimbizi hawa toka Burundi wanapata chakula cha kutosha kwaajili ya mahitaji yao.

4
Mkimbizi Irene Ntibelenda (katikati) akiwa pamoja na ndugu yake Sengiyu Mvajeme (kulia) wakiwa wamebeba mgao wa chakula.

5
Wakimbizi wakifunga shehena ya mahindi.

6
Sehemu ya shehena ya chakula ukiwepo unga wa mahindi na mafuta ya kupikia ikiwa katika ghala la kuhifadhia chakula. 

(PICHA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI – WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI)

No comments

Powered by Blogger.