Header Ads

MTANGAZA NIA YA URAIS, EDWARD LOWASSA AANZA KUSAKA WADHAMINI KANDA YA ZIWA

Pichani, Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, ambaye tayari amechukua fomu za kuomba CCM imteue kuwania urais, Edwrad Lowassa, akipungia mkono maelfu ya wanachama wa chama hicho na wananchi wengine baada ya kupata wadhamini kwenye ofisi ya CCM wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza Ijumaa Juni 5, 2015. 

KUTOKA MWANZA

MAELFU ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM, na wakazi wengine wa jiji la Mwanza, leo Ijumaa Juni 5, 2015, walifurika kwa wingi kwenye ofisi za CCM wilaya ya Nayamagana na ile ya Ilemela, wengine wakitaka kumuona na kupeana mikono na wengine kwa nia ya kumdhamini Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edwrad Lowassa, alipofika jijini Mwanza kutafuta wana CCM wa kumdhamini katika safari yake ya Matumaini.

Madereva texi, waendesha bodaboda, na hata wafanyakazi na wasafiri kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza, waliacha shughuli zao kwa muda ili walau wamuone mtangaza nia huyo wa nafasi ya jurasi kupitia CCM.
Lowassa alichukua fomu, za kuomba kuteuliwa na CCM kuwania urais wa Tanzania, Alhamisi Juni 4, 2015 pale makao makuu ya CCM, na safari yake ya kusaka wadhamini ilianza “chap chap” pale pale Dodoma, na Mwanza ndio kituo cha kwanza nje ya Dodoma, ambacho Lowassa, ameanza kampeni yake ya kusaka wadhamini.


Lowassa, akipokea fomu za wadhamini ambazo tayari zimejazwa na wana CCM wilaya ya Ilemele, kutoka kwa Katibu wa CCM wilayani humo, , Loti Olele Mtui Lazaro
Mmoja wa madereva Texi, akionyesha bango la kumuunga mkon o Lowassa, katika safari ya matumaini 2015
Lowassa, akipokea fomu zilizojazwa na wadhamini ambao ni wanachama wa CCM, kutoka kwa Katibu wa CCM wilaya ya Nyamagana, mkoani Mwanza, Elias Mpanda

Mwanachama mkongwe wa CCM, Mzee Rutaraka, akitoa salamu zake kwa niaba ya wazee jijini Mwanza

Watoto wa Chipukizi kutoka Chama Cha Mapinduzi, jijini Mwanza, Marie Kighei Joseph, (wapili kulia) na Sarafina Magabe, wakimkabidhi zawadi ya maua ikiwa ni ishara ya kumkaribisha Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowasa, alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwnza, Ijumaa Juni 5, 2015, ili kuomba wadhamini baada ya kuchukua fomu za kuomba kuwania urais wa Tanzania kuputia CCM

Lowassa, akiteremka kutoka ndani ya ndege baada ya kuwasili jijini Mwanza kuomba wadhamini

Wananchi waliokuwa na kiu ya kumuona Lowassa, walilazimika kupanda juu ya viti kutokana na msongamano wa watu waliofurika kwenye mitaa jirani na odfisi za CCM wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza Ijumaa Juni 5, 2015

Wasafiri na wafanyakazi wa uwanja wa ndege wa Mwanza, waliacha shughuli zao ili walau wapate kumuona Lowassa, alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwnaza Ijumaa Juni 5, 2015, tayari kutafuta wadhamini


Lowassa, akionyesha fomu ambayo tayari imejazwa na wadhamini wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza


No comments

Powered by Blogger.