Header Ads

Spika wa Bunge JOB NDUGAI apokea Ujumbe Kutoka Bunge la Zambia

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Waheshimiwa Wabunge kutoka Bunge la Zambia ambao pia ni Wajumbe wa kamati ya Miundombinu kutoka Bunge hilo waliokuja kubadilishana uzoefu na kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu, katika kikao kilichofanyika leo Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kulia)akimkabidhi kitabu chenye Sheria Mbali mbali za Bunge Mhe. Douglas Syakalima (wa pili kushoto), ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ya Miundombinu na Kiongozi wa Msafara wa kutoka Bunge hilo, Wabunge hao wamekuja kubadilishana uzoefu na kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu katika kikao kilichofanyika leo Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma. Kushoto ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson na kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu Mhe. Prof. Norman Sigala King.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (Kaunda suti nyeusi katikati)akipiga picha ya pamoja na Waheshimiwa Wabunge kutoka Bunge la Zambia ambao pia ni Wajumbe wa kamati ya Miundombinu kutoka Bunge hilo waliokuja kubadilishana uzoefu na kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakiongozwa na Mhe. Douglas Syakalima, ambae ni Mwenyekiti wa Kamati na Kiongozi wa Msafara/Ujumbe huo katika kikao kilichofanyika leo Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.

No comments

Powered by Blogger.