Header Ads

Waziri wa Afya UMMY MWALIMU akagua Kambi ya Wagonjwa wa Kipindupindu ya NYANKUMBU Mkoani GEITA

Wananchi wa Mkoa wa Geita wameaswa kufuata kanuni za usafi wa mazingira ili kudhibiti maumbukizi ya ugonjwa wa kipindupindu,Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu mara baada ya kutembelea kambi ya kipindupindu iliyopo kwenye kituo cha afya cha Nyankumbu.

mli1
Waziri Ummy akivaa vifaa maalum vya kujikinga na kipindupindu kabla ya kuingia kwenye kambi hiyo,kulia ni Mganga mfawidhi wa Kituo hicho Josephat Msafiri.
(Picha Zote na Catherine Sungura WAMJW-GEITA).

mli2 
 Waziri Ummy akivua vifaa hivyo mara baada ya kutoka kuwasalimia wagonjwa wa kipindupindu waliolazwa kwenye kambi hiyo,wagonjwa waliopo hadi leo mchana ni wagonjwa wanne.

mli3 
  Waziri huyo akiongea na mmoja wa wagonjwa wa kipindupindu waliolazwa kwenye kambi.

  mli4 
  Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiwasalimia wagonjwa wa kipindupindu(hawapo pichani)kulia ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita Dkt.Joseph Kisala.

mli5 
  Baadhi ya wagonjwa wa kipindupindu waliolazwa kwenye kambi ya kituo cha afya cha Nyankumbu.

No comments

Powered by Blogger.