Header Ads

Siku ya Vijana Duniani Kuadhimishwa Kitaifa Mkoani SIMIYU

Frank Mvungi-Maelezo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi siku ya Kilele cha maadhimisho ya siku ya Vijana Kitaifa yatakayofanyika Mkoani Simiyu Oktoba 14 mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Antony Mavunde wakati wa mkutano na waandishi wa Habari.

Mhe Mavunde amebainisha kuwa Kauli mbiu ya Siku ya Vijana mwaka huu ni “Tokomeza umasikini kwa uzalishaji endelevu na matumizi yenye tija”.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri MkuuKazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe.Anthony Mavunde akiongea na waandishi wa Habari leo Jijijni Dar es salaam kuhusu maadhimisho ya siku ya Vijana Duniani inayoadhimishwa Kitaifa tarehe 14/10/2016,Mkoani Simiyu. 
Baadhi ya Waandishi wa habari wakifuatilia mkutano wa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe.Anthony Mavunde.

No comments

Powered by Blogger.