Hizi Dola 1,000,000 ni za Nani?.."Polisi Nchini ANGOLA yamsaka Mmiliki wake"
Polisi nchini Angola wanamtafuta
mmiliki wa mkoba uliopatikana kwenye ndege ukiwa na dola milioni moja
sawa na £650,000, ambao uliachwa kwenye ndege iliyokuwa ikisafiri hadi
mjini Beijing, Uchina.
Msemaji wa polisi Aristofanes dos Santos amesema kuwa uchunguzi sasa umeanzishwa kubaini asili ya pesa hizo ambazo zimetwaliwa na serikali.
Wachambuzi wanasema kuwa yeyote atakayedai kumiliki pesa hizo ataweza tu kurejesha asilimia 1.5% ya jumla ya pesa zote huku akikabiliwa na mashtaka ya kusafirisha pesa kinyume cha sheria.
Post a Comment