Header Ads

Serikali yaahidi Kukamilisha Miradi ya Vijana

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akiongea na Maafisa Vijana na kuwataka kutumia elimu na ujuzi walioupata katika mafunzo ya ujasiriamali na ubunifu katika kuisaidia serikali kutimiza dhamira yake ya kuwainua vijana kiuchumi, wakati wa hafla ya ufungaji wa mafunzo ya ujasiriamali na ubunifu kwa Maafisa Vijana jijini Arusha.

Mkurugenzi Mkuu wa Chuo cha Uongozi cha Mashariki na Kusini mwa Afrika (ESAMI) Prof Bonard Mwape akiwaeleza maafisa vijana kuhusu umuhimu wa kubadilisha fikra za vijana ili kuwawezesha kujiajiri kupitia mafunzo watakayowapatia ya ujasiriamali, wakati wa hafla ya ufungaji wa mafunzo ya ujasiriamali na ubunifu kwa Maafisa Vijana jijini Arusha.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akiwakabidhi Baadhi ya Maafisa Vijana vyeti vya kuhitimu mafunzo ya Ujasiriamali na ubunifu, wakati wa hafla ya ufungaji wa mafunzo ya ujasiriamali na ubunifu kwa Maafisa Vijana jijini Arusha.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akimueleza jambo Mkurugenzi Mkuu wa Chuo cha Uongozi cha Mashariki na Kusini mwa Afrika (ESAMI) Prof.Bonard Mwape wakati wa hafla ya ufungaji wa mafunzo ya ujasiriamali na ubunifu kwa Maafisa Vijana jijini Arusha.

No comments

Powered by Blogger.