Muda wa Kujisajili Mahujaji Wasogezwa Mbele
Naibu Mwenyekiti Ofisi Kuu ya Hijja Tanzania (BIITHA), Yusuf Musun (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu kusogezwa mbele muda wa kujisajili kwenda Hijja kutoka Juni 15 hadi Agosti 25 mwaka huu. Kulia ni Ofisa Habari wa Biitha, Hamisi Tembo na Mratibu wa Biitha, Abdallah Khalid.
Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.
Na Dotto Mwaibale
MAHUJAJI nchini wametakiwa kujitokeza kujisajili katika
taasisi zilizosajiliwa kisheria ili kujiandaa kwenda katika ibada ya hija
itakayofanyika nchini Saud Arabia Septemba 16 mwaka huu.
Kauli hiyo imetolewa Dar es Salaam leo na Naibu Mwenyekiti
wa Ofisi Kuu ya Hijja Tanzania Bara na Zanzibar, Yusuf Musun
wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kusogeza muda huo
kutoka Juni 15 hadi Agosti 25 mwaka huu,
Alisema kusogeza mbele kwa muda wa usajili ni kutoa fursa
kwa wanaotarajia kwenda kuhiji ili waendelee kujitokeza kwa wingi kujisajili
katika taasisi zilizo rasmi.
Alisema wananchi wenye nia ya kwenda hijja lakini hawana fedha
za kulipa kwa mkupuo wanaweza kwenda kulipia kidogo kidogo kwenye ofisi husika.
Musun alisema lengo la kutoa mwito huo ni kuhimiza watu
wanaolipa fedha zao binafsi na wale wanaolipiwa na mashirika mbalimbali
kujisajili kwa wakati ili usajili uweze kumalizika katika muda uliopangwa.
"Waislamu wengi hawatoe hela zao kutoka mfukoni wengi
wao wanaolipiwa na mashirika mbalimbali hivyo tunawahimiza wajisajili kwa
wakati kwa ajili ya safari hiyo ya hijja.
|
Post a Comment