Header Ads

Mabondia LULU KAYAGE na RAMADHANI SHAURI kuzipiga Afrika Kusini Agosti 9

Mabondia Wa ngumi za kulipwa nchini Tanzania , Ramadhani Shauri na Lulu Kayage tarehe 07 mwezi huu wanaondoka nchini kwa ndege ya Ethiopia air line ,wakielekea nchini afrika kusini kwa ajili ya kuzipiga na mabondia Wa huko. 

Wakati msichana Lulu Kayage atazipiga na Lizbeth sivhaga  Shauri atazipiga na bondia mzoefu Philip ndlovu ambaye amshawahi kuzipiga na Floyd mayweather hapo mwaka 2003, mapambano hayo yatafanyika tarehe 09 Aug katika mji Wa Limpopo.

 awali mabondia hao wataongiozana na Rais wa TPBO Yassin Abdallah kwa  ndege Ethiopia air line bondia Lulu Kayage anakwenda kupambana uko baada ya kumtwanga Mwanne Haji kwa point mpambano wa raundi sita  na kupata nafasi hiyo.

 Kayage kwa sasa ni bondia nambari moja kwa upande wa wanawake katika uzito wake wa kg 51 lulu mpaka sasa ameshiliki mapambano 6 kasinda 4 kapigwa 1 na moja alitoka sale na bondia Halima Ramadhani.

No comments

Powered by Blogger.