DED Chamwino apewa wiki mbili kukamilisha mradi wa maji Manzase
Naibu
Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Selemani
Jafo akiwataka Viongozi wa Serikali kutumia vyema pesa za Mfuko wa Busket Fund
ambao ni mfuko wa fedha za Afya katika kuimarisha huduma bora ya Afya nchini
Naibu
Waziri Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo
akikagua kifaa cha kisasa cha kupimia macho katika hospitali ya Mvumi wakati wa
ziara yake ya kukagua huduma ya Hospitali Kimbizi inayohusisha Madaktari Bingwa
ambao wanatibu magonjwa mbalimbali Wilayani Chamwino. Kampeni hiyo itadumu kwa
muda wa siku tano kuanzia tarehe 15 Mei, 2017 hadi Mei 19, 2017
Naibu
Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa TAMISEMI selemani Jafo akiwa katika
picha ya pamoja na Viongozi wa Serikali, Madaktari Bingwa, Viongozi wa Dini na
Siasa katika Hospitali ya Mvumi.
....................................................................
Naibu Waziri Ofisi ya
Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI)Selemani Jafo amemtaka
Mkurugenzi wa Wilaya ya Chamwino Athuman Masasi kuhakikisha kuwa Mradi wa maji
wa kijiji cha Manzase unamalizika ifikapo mwishoni mwa mwezi mei, mwaka huu.
Jafo ameyasema hayo
alipokuwa anafanya ziara yake katika hospitali ya Mvumi ambapo amezindua huduma
ya Hospitali Kimbizi inayohudumiwa na Madaktari Bingwa ambao watatoa huduma ya
kitabibu kwa siku tano kuanzia leo, tarehe 15 hadi Mei 19, 2017 wilayani humo.
Madaktari hao bingwa
watatibu magonjwa ya ndani kwa watu wote, watoto, mifupa, masikio, pua na koo,
meno, upasuaji na magonjwa ya uzazi kwa upande wa akinamama.
Mbali na hilo pia, amesema katika sehemu
mbalimbali alizopita kumekuwa na changamoto ya kukosa huduma bora katika vituo
vya Afya kutokana na urasimu walionao Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za
Mitaa na kufanya Wananchi wengi wasio na uwezo wa kupata huduma hizo katika
kipindi cha nyuma na kwa kipindi hiki Serikali
imeshatoa ufumbuzi ambao Viongozi mnapaswa kuzitumia vyema pesa za Miradi ya
Afya kama Busket Fund katika kuboresha huduma za Afya kwa Wananchi wote.
Aidha Jafo amewataka
Wananchi kushiriki kikamilifu katika kupata huduma hizo kutoka kwa Madaktari
bingwa waliotoka katika hospitali mbalimbali nchini kwani huduma hizo
zinapatikana kwa bei nafuu na kutoka kwa Madaktari bingwa wenye uzoefu mkubwa
na wa muda mrefu.
Amepongeza ushirikiano
uliopo wa Mganga Mkuu wa Dodoma Dk.James Kiologwe Mbunge wa Jimbo la Mtera,
Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, wadau mbalimbali
pamoja na Kanisa la Anglikana kwa kuweza kuendesha zoezi hilo la huduma.
Akihitimisha hotuba
yake iliyojaa maelekezo ya Serikali, Jafo amesema baada ya zoezi hili
kukamilika ingependeza madaktari bingwa wote walioshiriki zoezi hili katika Wilaya
zote za Dodoma waje kujipongeza mjini Dodoma na kuwa mfano bora wa kuigwa kwa
kuwa zoezi hili ni zoezi la kwanza kufanyika nchini na likiwa limefanyika
mkoani Dodoma.
Post a Comment