Header Ads

M'barikiwa Irene Stefani atambuliwa Kenya


Mabaki ya M'barikiwa mtawa wa kale kutoka Italy IRENE STEFANI






Maelfu ya Wakatoliki wanahudhuria sherehe mjini Nyeri, Kenya, ya kum'bariki mtawa wa kale kutoka Italia. Irene Stefani aliwasaidia majeruhi wa Afrika Mashariki, wakati wa vita vya kwanza vya dunia, kabla ya kufariki kutokana na tauni mwaka 1930. 

Mabaki ya mtawa huyo yatasafirishwa hadi kanisa kuu la Nyeri siku ya jumapili. Wakatoliki wanaamini kuwa alionyesha miujiza baada ya kufa, katika mwaka wa 1989, pale watu waliokuwa wakikimbia vita vya Msumbiji, walipoomba kwa jina lake.

Wanasema maji yalitiririka kutoka mbele ya kanisa, na kunusuru maisha ya waliokuwa na kiu.

Wakatoliki nchini kenya wakongamana kwenye mji wa nyeri ili kum'bariki mtawa wa kale IRENE STEFANI ( Chanzo BBC Swahili )


No comments

Powered by Blogger.